Skip to Content

NAKUSHUKURU MUNGU WANGU

12 Mei 2026 na
NAKUSHUKURU MUNGU WANGU
Sr. Violet Kwanungu LSOF

Ee Mungu wangu, nakushukuru kwa zawadi ya uhai na kwa kuniumba katika upendo wako. Nakushukuru kwa macho uliyonijalia ambayo kupitia hayo ninaweza kuona uzuri na changamoto za dunia inayonizunguka. Nakushukuru kwa masikio yangu yanayonisaidia kusikia sauti, maneno, na mambo mbalimbali ya furaha na huzuni.

Nakushukuru kwa pua uliyonipa inayoniwezesha kutambua kila aina ya harufu nzuri na nyinginezo. Nakushukuru kwa mikono yangu inayoniwezesha kufanya kazi, kuhudumia wengine, na kutimiza majukumu mengi kila siku. Nakushukuru kwa miguu yangu inayoniwezesha kwenda popote ninapohitaji kwenda na kunisaidia kutembea katika safari ya maisha.

Nakushukuru, Mungu, kwa hekima na ufahamu ulioweka akilini mwangu, vinavyoniwezesha kufikiri vizuri na kufanya maamuzi sahihi. Nakushukuru kwa moyo unaodunda ndani yangu kwa uaminifu, ukiupa mwili wangu wote uhai. Nakushukuru kwa figo na kila kiungo ulichoumba ndani yangu, kila kimoja kikifanya kazi yake ya pekee kunifanya niendelee kuwa hai na mwenye afya.

Zaidi ya yote, nakushukuru kwa kila sehemu ya mwili wangu na kwa kila baraka uliyonijalia. Nisaidie daima kuona thamani ya zawadi hizi, ili niweze kuendelea kukusifu, kukuheshimu, na kukushukuru siku zote za maisha yangu. "Nitakushukuru kwa kuwa nimeumbwa Kwa jinsi ya ajabu ya kutisha.Matendo yako ni ya ajabu, na nafsi yangu yajua sana." (Zaburi 139:14)
 


katika Blogu yetu
NAKUSHUKURU MUNGU WANGU
Sr. Violet Kwanungu LSOF 12 Mei 2026
Shiriki posti hii
Lebo
Maktaba