"Nafsi yangu yamngoja Mungu peke yake kwa kimya, wokovu wangu hutoka kwake." (Zaburi 62:1) Jifunze kuwa kimya katika maisha yako; kwa kujifunza kuwa kimya utaepuka mambo mengi maishani mwako, na moyo wako utaendelea kuwa na amani.
Jifunze kuwa kimya ili uweze kutoa nafasi kwa akili yako kufikiri zaidi.
Jifunze kuwa kimya ili upate muda wa kusikiliza moyo wako.
Jifunze kuwa kimya ili uweze kusikiliza mawazo yako.
Jifunze kuwa kimya ili uweze kuleta utulivu kwa moyo wako.
Jifunze kuwa kimya na kuzungumza na nafsi yako ya ndani.
Jifunze kuwa kimya ili kugundua udhaifu wako.
Jifunze kuwa kimya ili kugundua nguvu zako, zungumza kidogo, fikiria zaidi.
JIFUNZE KUNYAMAZA
11 Februari 2026
na
Sr. Violet Kwanungu LSOF
katika Blogu yetu
Sr. Violet Kwanungu LSOF
11 Februari 2026